OVERCOMERS POWER CENTRE WAMPONGEZA
MH. EDWARD LOWASA NA UJUMBE WAKE KWA MCHANGO WAKE WA UJENZI WA KANISA NA KITUO CHA REDIO
Ni jambo la msingi na la hekima kumshukuru Mungu kwa kila
jambo jema linapofanikwa huku tukiona kwa macho haya mya kawaida lakini pia
tukiuona mkono wa mungu ukiwa upane wetu,kwanza kabisa tunamshukuru Mungu kwa
yote yaliyofanyika haikuwa kazi rahisi sana kufikia tulipofikia ilikuwa ni kazi
ngumu ilikuwa na vikwazo vya kila aina pamoja na hayo yote Mungu alitupigania
tutakuwa si wingi wa fadhira tusipo washukuru ndugu,jamaa na marafiki zetu
katika kristo bwana wetu kwa ushirikiano wao usioelezeka wala usio kuwa na
kipimo katika kufanikisha siku ya harambee ya ujenzi wa kanisa na kituo cha
redio Overcomers fm na kwa mapokezi mazuri kwa mgeni wetu waziri mkuu mstafu
Edward Lowasa aliye ongoza harambee hiyo.
Haikuwa kazi rahisi kama unavyoweza kufikiri juu ya ujio wa
mheshimiwa Edward Lowasa katika mkoa wa iringa katika kanisa la Overcomers
Power Centre kwaniaba ya kamati ya maandalizi ya tukio hilo Askofu wa kanisa
hilo Dk.Boaz Sollo amesema ni makusudi ya Mungu pekee kufanikiwa kwa tukio la
ujio wa Waziri mkuu mstaafu Mh.Edward Lowasa ili kuongoza harambee ya ujenzi wa
kanisa na kituo cha redio anasema kipekee kabisa aliweza kutoa shukurani zake
kwa makundi mbalimbali yaliyojitokeza katika ibada ya changizo.
Miongoni mwa kauli nzuri zilizotolewa na Askofu wa kanisa
hilo Dk Boaz Sollo alisema miongoni mwa malengo ya harambe hiyo ni ujenzi wa
kanisa na kituo cha redio ambavyo vitahakikisha watu wa mkoa wa Iringa na nchi
nzima wanabadilishwa mitazamo ya kidunia na kuachana na kumgeukia mungu lakini
pia ni kuwa kanisa litakalohakikisha watu wa mkoa wa Iringa wanapata
mafundisho ili kujikwamua kiuchumi kiroho na pia ni kutengeneza mahusiano mazuri
ya kiroho na waumini wa madhebu mengine hasa kupitia kituo cha Redio ya Kanisa
hilo iitwayo OVERCOMERS FM ambayo ni maarufu katika mikoa ya nyanda za juu
kusini inayopatikana katika masafa ya 98.6 Iringa.
Huduma inayotolewa na kanisa la Overcomers Power Centre itafanyika Baraka kubwa zaidi kwa wakazi wa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla na hii inajidhihirisha kutokana na jinsi watu walivyojitokeza katika siku ya uchangiaji iliyofanyika siku ya jumapili ya tarehe 21.04.2013 mkoni Iringa hivyo askofu Boaz pia aliwataka wakazi wa Iringa kutambua kuwa uwepo wa huduma hiyo nyanda za juu kusini ni kwa manufa yao hasa katika huduma ya kiroho.
Huduma inayotolewa na kanisa la Overcomers Power Centre itafanyika Baraka kubwa zaidi kwa wakazi wa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla na hii inajidhihirisha kutokana na jinsi watu walivyojitokeza katika siku ya uchangiaji iliyofanyika siku ya jumapili ya tarehe 21.04.2013 mkoni Iringa hivyo askofu Boaz pia aliwataka wakazi wa Iringa kutambua kuwa uwepo wa huduma hiyo nyanda za juu kusini ni kwa manufa yao hasa katika huduma ya kiroho.
Ili kuthamini michango
inayotolewa na viongozi mbalimbali hapa nchini katika kuhakikisha kazi ya mungu
inasonga mbele Kanisa la Overcomers Power Centre Iringa chini ya mtumishi wa
Mungu Askofu Dk Boaz Sollo lilimkabidhi
tuzo maalum na kumtunuku Waziri
mkuu aliyejihuzuru Mh Edwadi Lowasa ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika
harambee hiyo .
Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hiyo Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo amesema
kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo wa nchi katika kuyasaidia makanisa pamoja
na shughuli za kijamii wameona ni vyema kumtunuku tuzo ya Heshima ili kumtia
moyo kwa kazi anayo ifanya kwa jamii pamoja na changamoto nyingi anazokutana
nazo wakati wa kujitolea na kusaidia suala la maendeleo katika jamii hasa wale
wanao mpinga katika hilo ili kumkatisha tamaa hivyo Askofu Boaz Sollo pamoja na
waumini wa kanisa hilo wataendelea kumuombea ili afanikiwe zaidi pamoja na
kushinda vikwazo vinavyomkabili kiongozi huyo.
"tunatambua mchango wako kwa jamii na umesaidia makanisa mengi wau wengi pamoja na vikundi vingi kwakweli umefanyika kuwa mtu wa watu kwa kuliona hilo tumeona tukutunuku Tuzo ya heshima ili kumtia moyo na usikate tamaa kuendelea kuwasaidia watu mbalimbali pale wanapomuhitaji"
"tumeona mchango wake na tumeguswa na hilo sisi tutendelea kumuombe kwa Mungu ili afanikiwe katika yale anayoyafanya hata kama kuna watu wanaompinga hii inatokana kwamba siku zote tunaamini shetani hapendi maendeleo ya mtu wa Mungu"alisema askofu.
Katika harembee hiyo zaidi shilingi Mil 70 zilipatikana kutokana na michango iliyotolewa na wadau mbalimbali wakati mgeni rasmi akichangia sh mil 15 ambapo aliambatana na ujumbe wa watu wa nne ambao ni mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe,Kange Lugola,Mendrad Kigola Mbunge wa Mufindi kusini pamoja na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Litha Kabati. Kwaniaba ya kamati ya askofu Boaz aliwashukuru wale wote walioshiriki.
"tunatambua mchango wako kwa jamii na umesaidia makanisa mengi wau wengi pamoja na vikundi vingi kwakweli umefanyika kuwa mtu wa watu kwa kuliona hilo tumeona tukutunuku Tuzo ya heshima ili kumtia moyo na usikate tamaa kuendelea kuwasaidia watu mbalimbali pale wanapomuhitaji"
"tumeona mchango wake na tumeguswa na hilo sisi tutendelea kumuombe kwa Mungu ili afanikiwe katika yale anayoyafanya hata kama kuna watu wanaompinga hii inatokana kwamba siku zote tunaamini shetani hapendi maendeleo ya mtu wa Mungu"alisema askofu.
Katika harembee hiyo zaidi shilingi Mil 70 zilipatikana kutokana na michango iliyotolewa na wadau mbalimbali wakati mgeni rasmi akichangia sh mil 15 ambapo aliambatana na ujumbe wa watu wa nne ambao ni mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe,Kange Lugola,Mendrad Kigola Mbunge wa Mufindi kusini pamoja na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Litha Kabati. Kwaniaba ya kamati ya askofu Boaz aliwashukuru wale wote walioshiriki.







