ASKOFU BOAZ SOLLO ATUMIA JINA LA YESU KUKOMESHA MAPEPO, IMANI ZA KISHIRIKINA KATIKA SHULE YA MSINGI ILALA
Friday, May 11, 2012
Thursday, April 26, 2012
![]() |
| Umati wa wakazi wa Iringa waliofika mbele kwaajili ya kuokoka na kuombewa na Askofu Dr Boaz Sollo |
| Mmoja wa waliopokea muujiza baada ya kuombewa akitoa ushuhuda mbele ya kanisa kulia Askofu Sollo akimsikiliza. |
| Askofu Boaz sollo akiongea na waumini OPC na wenye shida mbalimbali waliofika katika siku hii maalumu kwa maombi ya mtu mmoja mmoja. |
| Askofu Dr Boaz Sollo akifungua kwa maombi kabla hajaanza kuombea mwenye uhitaji mmoja mmoja aliyehudhuria katika ibada hiyo ya maombezi wengi walifunguliwa. |
| Congregation at IDYDC Hall |
ONE TO ONE PRAYER MIRACLE AT IDYDC HALL IRINGA
With Bishop Boaz Sollo of Endtime and OVERCOMERS POWER CENTER.
Many get healed and released from satan strongholds.
Naye Askofu Boaz Sollo aliwaasa kwa wale wanaofika katika ibada hizo kwaajili ya kuombewa na kuondoka kutofanya hivyo kwani. Baada ya kuponywa wanatakiwa wapate masomo ambayo yatawaimarisha katika Imani na kuwa na nguvu za kukabiliana na shetani.
Katika maombi hayo yaligawanywa kwa makundi mbalimbali wakiwemo watoto wadogo kuanzia miaka 13 ambao wanapigwa vita sana na shetani na mara nyingi watoto wamejikuta na watoto kutokana na kukosa nguvu ya Roho wa Mungu na kukosa maadili au malezi bora, Pia kabla ya kuwaombea aliwataka wototo wote wenye simu na walio katika mahusiano ya kimapenzi kufuta namba za wapenzi hao na kuzingatia malengo yao ya kimaisha.
Kundi lingine ni Wenye vizuri vya ukimwi, wasio na watoto, wenye vifafa na degedege pamoja na wamama wajawazito.
Askofu Dr Boaz Sollo wa makanisha
ya Endtime Harvest church (EHC) na kituo cha maombezi Overcomers Power Center
(OPC) wiki hii amendaa huduma ya maombezi kwa mtu mmoja mmoja ambayo itafanyika
katika ukumbi wa IDYDC mkoa wa Iringa.
Ibada hizo ambazo hufanyika kila
siku ya Alhamisi na Jumapili kuanzia saa nane hadi 12 jioni zimekuwa zenye
mafanikio kutokana na watu kufunguliwa katika vifungo vya shetani na kuponywa
magonjwa yalio gumzo kutokana na kutokuwepo na matibabu kama Ukimwi na
mengineyo.
Katika siku ya alhamisi ya leo
katika maombi ya mtu mmoja mmoja baada ya maombi hayo kijana Ansidal Ngoi (17)
kutoka Welu mkoani Iringa anashuhudia kuponywa kabisa kifafa ambacho kilianza
msumbua toka alipokuwa na miaka mitatu. Ngoi aliendelea kuweleza kuwa alijikuta
akishambuliwa na kifafa hicho mara tatu au tano kwa siku nakueleza kuwa ni
mwezi mmoja umepita na hali hiyo haijarudia tena. Amewataka wote wenye matatizo
na shida mbalimbali kutosita kufika katika huduma ya OPC kwa maombezi kwani ni
kweli kwamba Askofu Sollo anaye Mungu wa kweli.
Naye kijana Philipo Stephano toka
Misele anashuhudia kuwa mwaka 2007 alipima afya akagundulika kuwa ana Ukimwi
lakini baada ya kuombewa na Mtumishi wa Mungu ndipo alipochukua hatua ya kupima
tena majibu yalionesha kuwa hana ukimwi.
Mama aliyekuwa mjamzito na sasa
anamtotowa kiume kwa jina Joshua anatoa ushuhuda kuwa alianza kuhudhuria katika
huduma hiyo toka miezi mitatu iliyopita. Katika ujauzito aliokuwa nao ulimletea
matatizo ya kila mara lakini kutokana na huduma ya maombi alipata uponyaji.
Wakati wa kujifungua ulifika lakini siku ziliendelea kupita ndipo tena
alipoombewa akapata dalili ya uchungu na alipofika hospitali akajifungua
salama.
Thursday, April 12, 2012
OPERATION CHRISTMAS CHILD OCC YATOA ZAWADI IRINGA
Shirika la kimataifa linalohudumia watoto walio katika mazingira walio katika mazingira magumu jana kupitia muwakilishi wa shirika hilo hapa Nchini kwa mkoa wa Iringa Dr Boaz Sollo aliongoza zoezi la ugawaji wa zawadi kwa watoto.Zoezi hilo la ugawaji wa zawadi lilifanyika katika ukumbi wa IDYDC Mkoani wa Iringa ambapo watoto walikusanyika pamoja na viongozi mbalimbali wa kanisa kama wawakilishi na kukabidhiwa zawadi hizo.
Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi kwa niaba ya mwenyekiti wa OCC kitaifa Askofu Rodrick Mbwambo, Dr Bishop Boaz Sollo ambaye ni msimamizi wa makanisa ya ENDTIME HARVEST CHURCH na OVERCOMERS POWER CENTER(OPC), alieleza kuwa historia ya ugawaji zawadi hapa nchini umeanza kwa kipindi cha miaka kumi kwa sasa.
Dr Sollo ameongeza kuwa OCC inapeleka zawadi katika nchi 130 duniani kote ikiwemo Tanzania, huku kwa mkoa wa iringa ukiwa ni mwaka wa tatu toka zawadi hizi zianze kugawiwa kwa watoto wasiojiweza na wanaoishi katika mazingira magumu. Aliongeza kuwa zawadi hizo zinatolewa kupitia makanisa yote Iringa yaliyotayari kushirikiana na kamati ya OCC mkoani Iringa.
Mwaka huu koa wa iringa umeongezewa idadi ya mabox ya zawadi kutoka 3500 mwaka jana hadi 6,500 ambapo box moja lina thamani ya Tsh 30,000 na kufanya zawadi hizo kwa mkoa wa iringa kuwa na thamani 111,000,000.
Mbali na iringa OCC imefanikiwa kupeleka zawadi hizi mikoa ya Mwanza, Kilimanjaro,Mbeya, Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Huku kukiwa na matarijio ya kupata zawadi mara mbili zaidi ili kuwezesha kufikia wilaya zote za mkoa wa Iringa na mingineyo.
Dr Sollo aliishukuru Serikali kwa kusamehe kodi ya ushuru kwa makontena ya zawadi na kuomba serikali ya Tanzania kutumia mamlaka ya bandari kuweka mfumo rahisi wa kutoa zawadi wa kutoa vitu bandarini kwani kila kila mwaka wanalazimika kulipa mamilioni ya fedha yajulikanayo kama "storage charge".
Pia Dr Sollo alitoa tahadhari kwa serikali kuwa makini kwa yeyote atakayejaribu kuhatarisha amani kwa kutumia dini au siasa.
Naye muwakilishi wa Mgeni rasmi Joseph Nyikani afisa elimu mkoa wa iringa alitoa shukrani kwa uongozi wa OCC kwa kuutambua umuhimu na kumualika Mkuu wa mkoa Dr. Christine Ishengoma kuwa mgeni rasmi. Aliweka msisitizo kwa watoto ambao wengi ni wanafunzi kuzingatia Elimu kwani elimu ndio msaada mkuu katika maisha yao ya sasa na baadae.
Aliongeza kuwa kwa kuwa mbali na OCC kutoa zawadi inatoa elimu ya maadili ambapo maadili mengi yameonekana kushuka kutokana na elimu hiyo kupuuziwa na kutoa wito kwa wazazi kuwafunza watoto wao ili taifa liwe lenye maadili maana mmomonyoko wa maadili unapoteza sifa ya taifa.
Monday, March 19, 2012
THE CERTIFICATE AWARDED TO BISHOP DR,BOAZ SOLLO FROM JAPAN BIBLE INSTITUTE
Taasisi ya Biblia ya Japan imemntunuku Askofu Boaz Sollo Shahada ya udaktari wa falsafa ya Theolojia Doctorate degree in Divinity.
Askofu Sollo amehitimu masomo ya Theolojia katika Taasisi hiyo, kwa sasa jina lake ni Askofu Dr. Boaz Sollo.
Askofu Sollo amehitimu masomo ya Theolojia katika Taasisi hiyo, kwa sasa jina lake ni Askofu Dr. Boaz Sollo.
Wednesday, March 14, 2012
MATENDO MAKUU YA YESU YAONEKANA MBEYA GOSPEL CRUSADE
Mbali na miujiaza mingi kutendeka moja ya muujiza ulioshangaza maelfu ya watu waliohudhuria katika mkutano wa injili wa huduma ya overcpmers power center na kanisa la Endtime Harvest Church inayoongozwa na Askofu Dr Boaz Sollo ni neno la mamlaka alilotoa kuamuru mvua isinyeshe hadi mkutano huo ulipomalizika.
Mkutano huo uliofanyika hivi karibuni katika viwanja vya uhasibu jijini mbeya na kuhudhuriwa na maelfu ya wakazi wa jiji hilo na mikoa ya pembezoni.
Pamoja ni kwamba ni majira ya masika, kwa siku tatu za mkutano huo uliovuta watu wengi kwa Yesu Kristo na kuokoka baada ya kuponywa magonjwa sugu, mvua ilisimama nyakati za jion na kunyesha usiku na asubuhi jambo ambalo askofu Boaz alisema lilidhihirisha jinsi Mungu anavyojibu maombi.
Subscribe to:
Posts (Atom)
