WELCOME TO BOAZ FOUNDATION TANZANIA

OVECOMERS POWER CENTER, ENDTIME HARVEST CHURCH,OVERCOMERS FM RADIO IRINGA,OVERCOMERS MINISTRY TO THE NEEDY.

Thursday, April 25, 2013

OVERCOMERS POWER CENTRE WAMPONGEZA 
MH. EDWARD LOWASA NA UJUMBE WAKE KWA MCHANGO WAKE WA UJENZI WA KANISA NA KITUO CHA REDIO 



Ni jambo la msingi na la hekima kumshukuru Mungu kwa kila jambo jema linapofanikwa huku tukiona kwa macho haya mya kawaida lakini pia tukiuona mkono wa mungu ukiwa upane wetu,kwanza kabisa tunamshukuru Mungu kwa yote yaliyofanyika haikuwa kazi rahisi sana kufikia tulipofikia ilikuwa ni kazi ngumu ilikuwa na vikwazo vya kila aina pamoja na hayo yote Mungu alitupigania tutakuwa si wingi wa fadhira tusipo washukuru ndugu,jamaa na marafiki zetu katika kristo bwana wetu kwa ushirikiano wao usioelezeka wala usio kuwa na kipimo katika kufanikisha siku ya harambee ya ujenzi wa kanisa na kituo cha redio Overcomers fm na kwa mapokezi mazuri kwa mgeni wetu waziri mkuu mstafu Edward Lowasa aliye ongoza harambee hiyo.

Haikuwa kazi rahisi kama unavyoweza kufikiri juu ya ujio wa mheshimiwa Edward Lowasa katika mkoa wa iringa katika kanisa la Overcomers Power Centre kwaniaba ya kamati ya maandalizi ya tukio hilo Askofu wa kanisa hilo Dk.Boaz Sollo amesema ni makusudi ya Mungu pekee kufanikiwa kwa tukio la ujio wa Waziri mkuu mstaafu Mh.Edward Lowasa ili kuongoza harambee ya ujenzi wa kanisa na kituo cha redio anasema kipekee kabisa aliweza kutoa shukurani zake kwa makundi mbalimbali yaliyojitokeza katika ibada ya changizo.

Miongoni mwa kauli nzuri zilizotolewa na Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo alisema miongoni mwa malengo ya harambe hiyo ni ujenzi wa kanisa na kituo cha redio ambavyo vitahakikisha watu wa mkoa wa Iringa na nchi nzima wanabadilishwa mitazamo ya kidunia na kuachana na kumgeukia mungu lakini pia ni kuwa kanisa litakalohakikisha watu wa mkoa wa Iringa wanapata mafundisho ili kujikwamua kiuchumi kiroho na pia ni kutengeneza mahusiano mazuri ya kiroho na waumini wa madhebu mengine hasa kupitia kituo cha Redio ya Kanisa hilo iitwayo OVERCOMERS FM ambayo ni maarufu katika mikoa ya nyanda za juu kusini inayopatikana katika masafa ya 98.6 Iringa.

Huduma inayotolewa na kanisa la Overcomers Power Centre itafanyika Baraka kubwa zaidi kwa wakazi wa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla na hii inajidhihirisha kutokana na jinsi watu walivyojitokeza katika siku ya uchangiaji iliyofanyika siku ya jumapili ya tarehe 21.04.2013 mkoni Iringa hivyo askofu Boaz pia aliwataka wakazi wa Iringa kutambua kuwa uwepo wa huduma hiyo nyanda za juu kusini ni kwa manufa yao hasa katika huduma ya kiroho.

Ili kuthamini michango inayotolewa na viongozi mbalimbali hapa nchini katika kuhakikisha kazi ya mungu inasonga mbele Kanisa la Overcomers Power Centre Iringa chini ya mtumishi wa Mungu Askofu Dk Boaz Sollo lilimkabidhi  tuzo maalum na  kumtunuku Waziri mkuu aliyejihuzuru Mh Edwadi Lowasa ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo .

Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hiyo  Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo amesema kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo wa nchi katika kuyasaidia makanisa pamoja na shughuli za kijamii wameona ni vyema kumtunuku tuzo ya Heshima ili kumtia moyo kwa kazi anayo ifanya kwa jamii pamoja na changamoto nyingi anazokutana nazo wakati wa kujitolea na kusaidia suala la maendeleo katika jamii hasa wale wanao mpinga katika hilo ili kumkatisha tamaa hivyo Askofu Boaz Sollo pamoja na waumini wa kanisa hilo wataendelea kumuombea ili afanikiwe zaidi pamoja na kushinda vikwazo vinavyomkabili kiongozi huyo.

"tunatambua mchango wako kwa jamii na umesaidia makanisa mengi wau wengi pamoja na vikundi vingi  kwakweli umefanyika kuwa  mtu wa watu kwa kuliona hilo tumeona tukutunuku Tuzo ya heshima ili kumtia moyo na usikate tamaa kuendelea kuwasaidia watu mbalimbali pale wanapomuhitaji"

"tumeona mchango wake na tumeguswa na hilo sisi tutendelea kumuombe kwa Mungu ili afanikiwe katika yale anayoyafanya hata kama kuna watu wanaompinga hii inatokana kwamba siku zote tunaamini shetani hapendi maendeleo ya mtu wa Mungu"alisema askofu.

Katika harembee hiyo zaidi shilingi Mil 70 zilipatikana kutokana na michango iliyotolewa na wadau mbalimbali wakati mgeni rasmi akichangia sh mil 15 ambapo aliambatana na ujumbe wa watu wa nne ambao ni mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe,Kange Lugola,Mendrad Kigola Mbunge wa Mufindi kusini pamoja na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Litha Kabati. Kwaniaba ya kamati ya askofu Boaz aliwashukuru wale wote walioshiriki.

Thursday, March 28, 2013

UMOJA NI NGUVU HASA KATIKA WAKATI HUU AMBAO OVERCOMERS POWER CENTRE WAKIONYESHA JITIHADA ZAO ZA KUJENGA NYUMBA YA BWANA ENEO LA ZIZILANG'OMBE MANISPAA YA IRINGA NA HUU SIYO WAKATI WA KUKAA KWENYE NYUMBA ZENYE MAPAMBO HEKARU LA BWANA LINAHARIBIKA.

Kauli hii inajidhihirisha wazi katika kipindi hiki kigumu ambacho waumini wa kanisa la Overcomers Power Centre (OPC) wakikabiliwa na ujenzi wa nyumba ya Mungu kwa kutumia nguvu zao pamoja na muda wao kuhakikisha wanapata mahali pa kuabudia,Mchakato wa ujenzi wa kanisa hilo ulianza kwa kutafuta eneo la kujenga Hekaru hilo kwa kuchangia kiasi cha fedha ambazo waumini hao waliwiwa kutoa ili kusaidia ununuzi wa kiwanja cha ujenzi wa kanisa hilo haikuwa kazi rahisi kufikia mahali walipo fikia leo hata ukiangalia katika picha zilizowekwa hapo chini na hiyo ndiyo uhalisia wenyewe kwamba waumini hao wamedhamilia kumjengea Mungu Hekaru,

Miongoni mwa kauli nzuri zilizotolewa na Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo alisema miongoni mwa malengo ya ujenzi wa kanisa hilo ni kuhakikisha watu wa mkoa wa Iringa na nchi nzima wanabadilishwa mitazamo ya kidunia na kuachana na kumgeukia mungu lakini pia ni kuwa kanisa litakalohakikisha watu wa mkoa wa Iringa wana pata mafundisho ili kujikwamua kiuchumi kiroho na pi ni kutengeneza mahusiano mazuri ya kiroho na waumini wa madhebu mengine hasa kupitia kituo cha Redio ya Kanisa hilo iitwayo OVERCOMERS FM ambayo ni maarufu katika mikoa ya nyanda za juu kusini inayopatikana katika masafa ya 98.6 Iringa.

Huduma inayotolewa na kanisa la Overcomers Power Centre imefanyika Baraka kubwa kwa wakazi wa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla na hii inajidhihirisha kutokana na jinsi watu wanavyofunguliwa pia wanavyo barikiwa na kufanikiwa katika maisha yao.

Harambee ya uchangiaji fedha kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo.

Ili kuthamini michango inayotolewa na viongozi mbalimbali hapa nchini katika kuhakikisha kazi ya mungu inasonga mbele Kanisa la Overcomers Power Centre Iringa chini ya mtumishi wa Mungu Askofu Dk Boaz Sollo limeandaa tuzo maalum nayaheshima kwaajili ya kumtunuku Waziri mkuu aliyejihuzuru Mh Edwadi Lowasa ambaye ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo inayotarajiwa kufanyika tarehe 21/04/2013 hapo mkoani Iringa kwaajili ya ujenzi huo.

Akizungumzia kuhusu tuzo hiyo Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo amesema kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo wa nchi katika kuyasaidia makanisa pamoja na shughuli za kijamii wameona ni vyema kumtunuku tuzo ya Heshima ili kumtia moyo kwa kazi anayo ifanya kwa jamii pamoja na changamoto nyingi anazokutana nazo wakati wa kujitolea na kusaidia suala la maendeleo katika jamii hasa wale wanao mpinga katika hilo ili kumkatisha tamaa hivyo Askofu Boaz Sollo pamoja na waumini wa kanisa hilo wataendelea kumuombea ili afanikiwe zaidi pamoja na kushinda vikwazo vinavyomkabili kiongozi huyo.

"tunatambua mchango wake kwa jamii na amesaidia makanisa mengi wau wengi pamoja na vikundi vingi  kwakweli ni mtu wa watu kwa kuliona hilo tumeona siku hiyo ya Harambee tutamtunuku Tuzo ya heshima ili kumtia moyo na asikate tamaa kuendelea kuwasaidia watu mbalimbali pale wanapomuhitaji"

"tumeona mchango wake na tumeguswa na hilo sisi tutendelea kumuombe kwa Mungu ili afanikiwe katika yale anayoyafanya hata kama kuna watu wanaompinga hii inatokana kwamba siku zote tunaamini shetani hapendi maendeleo ya mtu wa Mungu"alisema askofu.

Kwa upande wa wananchi wa mkoa wa Iringa walipongeza kanisa hilo kwa kukumbuka kumpa tuzo kiongozi hiyo ambaye tangu ajihuzuru uongozi wake hakuwahi kufika Iringa na ameendelea kujitolea katika shughuli za jamii bila kubagua rangi au kabila la watu anaoweza kuwasaidia,hivyo wanamsubiri kwa hamu kubwa ili kumuunga mkono kwa shughuli atakayo ifanya ya kuongoza uchangiaji wa ujenzi wa nyumba ya bwana 

Haya ni majengo ya Ofisi pamoja na kituo cha redio ya Overcomers fm

Jengo hili la Ofisi za kanisa hilo pamoja na Kituo cha Redio
Mafundi wakiendelea na kazi ya Ujenzi wa ofisi za kanisa
Upende wa nyuma wa Ofisi
Upande wa mbele wa jengo la Ofisi na huo msingi mbele yake ndimo utakamopita ukuta wa kanisa lenyewe
Nguvu kazi ya waumini wa kanisa hilo la Overcomers Power Centre zikionekana hapo

Thursday, February 28, 2013

MKUTANO MKUBWA WA INJILI KUENDELEA KUTIKISA IRINGA KATIKA UWANJA WA SAMORA WAGONJWA WANAPONA,WALIOFUNGWA WANAFUNGULIWA NA KUWA HURU.

Askofu Dk.Boaz Sollo akihubiri katika mkutano wa Injili katika uwanja wa Samora Iringa
Askofu Dk.Boaz Sollo akiombea watu katika mkutano Iringa
Mamia ya wanairinga waliohudhuria mkutano

Wednesday, February 20, 2013

KUMBUKUMBU YA PICHA ZA MIKUTANO ILIYOFANYWA NA ASKOFU DK.BOAZ SOLLO KATIKA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI NI MIONGONI MWA MIKUTANO MIKUBWA ILIYOWAHI KUFANYIKA YENYE MIUJIZA MIKUBWA  NA BARAKA KWA WATU.

Askofu Dk.Boaz Sollo akiwaombea wenye shida katika mkutano

USIKOSE KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJIRI KATIKA UWANJA WA SAMORA



MKUTANO MKUBWA WA INJIRI IRINGA KUUNGURUMA KATIKA UWANJA WA SAMORA KUVUNJA NGUVU ZA KICHAWI.

Hizi ni siku kumi za miujiza mikubwa ambayo haijapatakutokea katika mkoa wa Iringa kuanzia terehe 23/03/2013 hadi tarehe 03/03/2013, ni katika mkutano mkubwa wa kuvunja na kuharibu nguvu za kichawi ambazo zimekuwa zikiwatesa watu kwa muda mrefu sasa zinakenda kukomeshwa ambapo maandalizi ya mkutano huo yamekamilika na Wahubiri wa kimataifa zaidi ya wanne watakuwepo kuwahudumia watu wa mikoa ya nyanda za juu kusini,ikiwa ni pamoja na mwenyeji wa mkutano Askofu Boaz Sollo, Mtume Ken Gitonga,Bonefasi Indeche pamoja na Dastan Maboya ambapo Askofu Dk.Boaz Sollo alithibitisha kwamba huu ni mkutano ambao haujawahi kufanyika iringa na aliwataka wakazi wa Iringa kushiriki kikamilifu katika mkutano huo ili waweze kuziona Baraka za Mungu katika maisha yao.
   
Wakati huohuo wakristo nchi wametakiwa kumtumaini mungu na siyo kuogopa nguvu za Kishirikina. 
Hayo yamesemwa na askofu wa huduma ya overcomers power centre pamoja na makanisa ya End Time And Havesting Church Dr.Boaz Sollo alipokuwa akifundisha katika ibada zilizofanyika mfululizo wiki iliyopita ikiwa ni moja ya masomo yanayoendelea kufundishwa na mtumishi huyo na kuwataka waumini wa kanisa hilo kutambua namna wanavyo weza kuzishinda nguvu za kichawi ambazo mara nyingi zimeonekana kuwasumbua watu wengi hususani katika mkoa wa Iringa.

Askofu Boaz aliwataka wazazi kutambua umuhim wa kuwalinda watoto wao kwa maombi ili kuwakinga watoto hao na nguvu za kichawi ambazo pia zimeendelea kuwatesa watoto huku wengine wakittumikishwa na kushughulishwa na shughuli za kishirikina lakini pia wengi wameshindwa kuendelelea na masomo kutokana na nguvu za kishirikina,hivyo a matendo ya mitume 13.6 akazungumzia habari za watu kama Bayesu au Elima aliyekuwa akimuhudumia liwali aliyekuja kuokoka na elima kufanya mbinu za kumfanya aache imani kwa hilo pia unaweza kuona jinsi wachawi wanavyofanyakazi ya kurudisha nyuma imani za watu waliomjua mungu kutokana na shuhuda mbalimbali ambazo watu wameweza kushudia na Mungu amejidhihirisha wazi kwamba kuna jambo ambalo mungu ametenda kwa watu wa Iringa kupiia huduma ya mtumishi wa Mungu Askofu Boaz solo,ikiwa bado somo hilo linalo husiana katika mkutano wa Samora Iringa.